Wednesday, December 15, 2010

UN kusaidia TZ dola 773 milioni za Marekani

Serikali ya Tanzania na Umoja wa Mataifa (UN) ,wamesaini makubaliano ya utaratibu mpya wa misaada unaojulikana kama UNDAP utakaodumu kwa miaka 4 kuanzia mwaka ujao wenye thamani ya dola 773 milioni za Marekani.

Makubaliano hayo yalifanyika jana, jijini Dar es Salaam ,baina ya serikali ya Tanzania na Umoja wa Mataifa , ukiwa na lengo la kuondoa umasikini nchini kwa kusaidia Mfuko wa MKUKUTA na MKUZA.


Hii ni mara ya kwanza serikali ya Tanzania na UN kufikia hatua ya kusaini makubaliano hayo ikiwa ni sawa na mkataba kati ya nchi ya Tanzania na UN kwa miaka minne.

Tukio hilo lilishuhudiwa na msaidizi wa Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na Uchumi, Ramadhani Khijjah na Alberic Kacou, kutoka UN jijini Dar es salaam.

Khijja alisema kuwa serikali ya Tanzania iko tayari kufanya kazi na UN na kweli ni kwamba kuna UN tu na si nyingine .

Alisema Tanzania haikuwa nyuma bali inajitahidi kupiga hatua kibiashara na huu mkataba unaonyesha ni namna gani Tanzania ilivyodhamiria kupiga hatua kimaendeleo.

Akizungumza kwa niaba ya wawakilishi wa Umoja wa Mataifa ,Balozi wa Ireland, Lorcan Fullam, alitoa pongezi kwa muungano huo wa serikali ya Tanzania na Umoja wa Mataifa akifafanua kwamba kinachoangaliwa zaidi ni nini kitafanyika kwa hiyo miaka minne ijayo kwa sababu sio mbali.

No comments:

Post a Comment